KUHUSU PUNYETO

Ni kwa kiwango gani upigaji punyeto huleta madhara? Hakuna upigaji punyeto uliyo salama na pia vilevile hakuna kiwango kilicho salama, licha ya kwamba mtu aliyefanya aliyejichua kwa kiwango kidogo ana nafasi ndogo ya kupata madhara. Hata hivyo, hakuna idadi maalumu inayoweza kuchukuliwa kama ni uchuaji au ufanyaji masturbation mkubwa au wa kupindukia (iliyovuka kiwango). Idadi ya kujichua (masturbation) anayoweza kufanya mtu bila madhara hutegemea afya ya mtu huyo na kemia ya mwili wake. Baadhi ya watu hupiga punyeto (masturbation) kwa muda mfupi katika kipindi fulani, mathalani mwezi mmoja tu au miwili. Na wengine wanaweza kufanya masturbation kwa muda mrefu kiasi cha mwaka mmoja au zaidi na hata huweza kufikia mara 2 hata mara 5 kwa siku, na wanaweza kufanya kila siku (NON STOP)! Kwa hakika huo ni upigaji punyeto uliyovuka mipaka, ni lazima itadhikisha ini na kazi za mfumo wa neva na lazima imweke mtu katika uhanisi hata kama ni kijana wa miaka 18, na kwa baadhi ya watu hata huweza kuwasababishia ugumba (yaani kushindwa kumtungisha mwanamke mimba)! Wanaume wengi sana walio na umri chini ya miaka 40 wana tatizo la kuishiwa nguvu za kiume kutokana na kujichua, yaani kupiga mgalala (masturbation). Ni wazi kwamba watu wengi wanapokuwa wanapiga punyeto, wanakuwa hawajui wanachokifanya, kama wangelijua basi wangeliichukia punyeto kama wanavyochukia ukoma! Hata baadhi ya watu wamediriki kunitumia meseji kutaka kujua uhusiano wa upungufu wa nguvu za kiume na punyeto, somo hili ni muafaka sana kwao sasa. Upigaji punyeto huleta mabadiliko makubwa katika mwili kama ambavyo nimeshagusia. Madhara ya mabadiliko hayo ndani ya kemia ya mwili yanaweza kujidhihirisha yenyewe kama uchovu, kupoteza nywele, kupoteza kumbukumbu, kuona ukungu, maumivu ya korodani/kinena, kufika kileleni haraka, kutoka kwa shahawa zenyewe, kushindwa kusimamisha uume vizuri, kukosa uzazi, maumivu ya mgongo/kiuno n.k. Naam! Hapa sasa tutazame madhara yanayoletwa kujichua (masturbation) ndani ya mwili, tutaangalia kwa ujumla kuhusu nguvu za kiume na vipengele vingine vya kiafya: Uume kusimama kwa uregevu Kama masturbation itafanywa sana kupindukia, huchochea kemikali iitwayo acetylcholine katika mfumo wa neva huria ubongo za parasimpathetiki (parasympathetic nerve). Hali hii inaweza kuzidisha sana kupita kiasi kiwango cha mchocheo, na matokeo yake itaweza kuzalisha sana kupita kiwango cha kawaida homoni zinazohusika na kujamiiana (sex hormones) na neurotransmitters kama vile acetylcholine, dopamine, serotonin na hivyo kusababisha mabadiliko ya kemia ndani ya mwili. Dopamine ni kemikali inayotengenezwa katika ubongo na iko katikati, na ni kipitisha ujumbe (neurotransmitter). Dopamine huhusika sana na raha. Kichocheo ambacho huzalisha aina yoyote ya mwitikio chanya pia vilevile huchochea utoaji wa dopamine katika ubongo. Uzalishaji huu mwingi wa kupita kiasi huenda moja kwa moja kudhoofisha mfumo wa viungo vinavyoshughulika na uzazi na tendo la ndoa. Na hatari yake kubwa ni kwamba, kama mtu hatatibiwa mapema, anaweza kuua nguvu za kiume kabisa na hata kujiletea ugumba. Parasympathetic nerve ni neva yenye jukumu la kusimamisha uume, kama mtu atafanya masturbation ya kupindukia, atazalisha kemikali nyingi ndani ya mwili, na uzalishaji huo hudhoofisha utendaji wa neva hii kwa kuifanyisha kazi kupita kiasi, na hivyo kwa baadaye uume wa mpiga punyeto unaweza kuwa unasimama kwa uregevu. Mfano wake ni kama umeme huu tunaoutumia majumbani mwetu kwa kazi mbalimbali (pengine tukitumia mfano wa umeme, msomaji anaweza kuelewa kwa urahisi zaidi). Ni kwamba, ndani ya miili yetu pia kuna umeme (bioelectricity). Unapofanya tendo la ndoa unazalisha umeme wa kawaida ndani ya mwili wako katika hali ya kawaida kwa sababu ni mwungano wa jinsia mbili tofauti, ni kama hasi na chanya. Lakini, unapofanya masturbation hali ni tofauti. Katika masturbation unazalisha umeme/kemikali nyingi sana, kwa sababu ‘unafosi’ umeme kutengenezeka kwa nguvu kwa kupitia chanya tu, umeme huo unaenda kuua vitu vinavyofanyiwa kazi na umeme huo. Ni kama ambavyo tumekuwa tukiona mara kwa mara umeme unapozidi majumbani mwetu, vitu ambavyo vilivyokuwa vikitumia umeme huo kama friji, tv, na kadhalika huungua. Katika miili yetu hali ni hivyo hivyo. Kwa hali hiyo, wapiga punyeto, watambue wanafanya jambo baya sana, watambue wanajiangamiza kwa mikono yao wenyewe. Madhara ya kuregea kwa uume kutokana na kujichua (masturbation), yanaweza kuanza kuonekana mapema au yanaweza kutokea baada ya muda mrefu, kutegemeana na afya ya mhusika na kemia ya mwili wake. Kufika haraka kileleni Upigaji wa punyeto au kujichua hupunguza sana nguvu za kiume na hata kuua kabisa nguvu hizo za kiume. Ni jambo ovu na hatari kabisa kwa afya ya mwanaume. Kudhoofika kwa neva huria ubongo za parasimpathetiki (parasympathetic nerve) husababishwa na upigaji punyeto wa kupindukia. Kama ambavyo nimekwishaeleza katika sehemu makala zingine, neva hii ndiyo yenye jukumu la kusimamisha uume, pia vilevile neva hii ndiyo yenye jukumu la kufunga milango ya shahawa kwa muda wa kutosha wa kufurahia tendo la ndoa. Pindi neva hii inapokuwa dhaifu, maji ya shahawa hutoka hata kama mtu yuko usingizini, wakati wa ndoto za mapenzi au hata wakati wa msisimko mdogo sana. Kwa nini mtu afike kileleni mapema kutokana na punyeto? Punyeto kama lilivyo tendo la ndoa, kama ambavyo tumeshaona huzalisha baadhi ya kemikali ndani ya ubongo (acetylcholine, serotonin, na dopamine) ambazo punde tu baadaye huleta raha ya akili na mwili. Kemikali hizi ni nzuri kwetu kwa sababu hutolewa katika kiwango maalumu. Hatari inakuja kwamba, kama zitazalishwa kwa wingi sana, zina tabia ya kukaa muda mrefu sana ndani ya mwili na kuzalisha madhara ya kimwili na kisaikololojia kama vile kutokuwa makini katika jambo, kupungua uwezo wa kukumbuka mambo, matatizo ya kukosa usingizi na mwili kukosa nguvu (physical lethargy). Pindi mtu anapopiga punyeto sana, huchochea seli zenye jukumu la uzalishaji wa homoni hizi. Seli hizi haziitiki tu kwa kuongeza utendaji wake wa kazi, bali pia idadi yake huongezeka kuliko kawaida, na hivyo mwili wa mpiga punyeto unakuwa na msisimko mkubwa sana, kiasi ambacho hata mwanamke anaweza kuvua nguo tu, na muathirika wa punyeto akajipizia mwenyewe! Jambo jingine baya ni kwamba, uzalishaji mwingi wa homoni hizi moja kwa moja huathiri neva ya parasimpathetiki (Parasympathetic nerve) yenye jukumu muhimu la kufunga milango ya maji ya shahawa kiasi cha mwanaume kufurahia tendo la ndoa na kuridhika na mwenza wake. Hivyo, neva hii inapoathirika, yaani inapokuwa regevu na ufikaji kileleni pia huathirika kwa kiwango kikubwa sana, kwa maana milango iko wazi, kufuli hakuna! Yaani neva inakuwa haina uwezo wa kufunga milango ya shahawa. Madhara mengine makubwa na hatari yanayoletwa na mpiga punyeto ni kwamba, tendo hili kwa kiwango kikubwa sana hudhuru kiungo muhimu sana kwa mwanaume kinachoitwa tezi-dume au tezi-shahawa (prostate gland). Kiungo hiki kiko chini ya kibofu cha mkojo. Baadhi ya kazi zake kubwa ni kutengeneza maji ya shahawa na ‘kukontroo’ shahawa. Kiungo hiki ndicho jeuri ya mwanaume, na pia tutakizungumza tena kwa urefu katika makala zetu za mbele. Kwa ufupi tu ni kwamba, prostate gland ndiye dreva; ndiye anayeamua kwamba hapa anafunga breki au hapana. Tezi hii ndiyo inayoamua kuwa sasa unafika kileleni au hapana. Wapiga punyeto huzalisha umeme mwingi ambao umeme huu huifanyisha kazi sana tezi hii na hivyo kuitanusha sana, na hivyo kuvimba. Inapovimba, ugonjwa ambao kitaalamu tunauita, Benign Prostate Hyperplasia (BPH), mpiga punyeto anakuwa anapata tatizo la kufika kileleni haraka, na hata umri utapokwenda zaidi anaweza kupata tatizo la mkojo kiasi cha kuhitaji kufanyiwa upasuaji. Pia, na kama mtu atafanya masturbation kabla ya kufikia umri wa miaka 21, ajue anajiua kabisa nguvu za kiume. Kwa sababu tezi hii katika wakati huu inakuwa katika ukuaji, inakoma kukua katika umri wa miaka 21. Hivyo, mpiga punyeto kabla ya muda huo anakuwa anavuruga ukuaji wake na kwa hiyo kujiletea uhanisi hasa kufika kileleni haraka mnoo! Inapovimba tezi hii huwa inapata msisimko mkubwa sana na inakosa kabisa ‘kuntroo ya shahawa’ (ya udhibiti wa shahawa). Hizo ndizo sababu zinazofanya wapiga punyeto wafike haraka sana kileleni. Wao wenyewe ni mashahidi, kilio chao kikubwa ni kufika keleleni haraka sana, ni kuingia tu na kumwaga! Utamkuta mtu ni kijana barobaro ambaye ukimwona unaamini akifanya mapenzi atachukua dakika 30 kufika kileleni, na hata zaidi hapo, na hata mke wake atamwamkia, “Shikamoo mume wangu!” Yaani anapewa heshima ya kipekee hata kama ana umri mdogo zaidi ya mke wake. Lakini ajabu barobaro huyu atakawambia anafika kileleni ndani ya dakika 1 au 2 au 3!! Huu tayari ni uhanisi! Hivyo mpiga punyeto aelewe kwamba anapofanya mchezo huo mchafu anaharibu milango yake ya shahawa, anadhuru tezidume, anadhuru misuli. Na hata baadhi ya wapiga punyeto uume huwa mdogo, au korodani kusinyaa na kuwa kama za mzee. Wapiga punyeto wamekuwa wakijiuliza kwa nini baadaye wamepata tatizo la ufikaji haraka kileleni? Kwa ufupi sababu zao ni hizo, hivyo matibabu yanapaswa yaanzie katika sababu hizo. Wasikurupike tu kubugia dawa, wanahitaji wapate mtaalamu aliyebobea katika mfumo wa mkojo na mfumo wa uzazi wa mwanaume, siyo kununua dawa mitaani. Vijana wanaosoma shule za kulala, na wanaopenda kutazama picha za ngono wana tabia hii sana ya kupiga punyeto, waelewe watakuja kukosa heshima ndani ya majumba yao punde muda tu watakapokuwa wako katikaya ndoa zao, ili wapate mahala pengine (kwa watu ambao hawajapiga punyeto) ili nao wastarehe na kufurahia tendo la ndoa. Kuna msemo usemao, “Usipofyeka msitu, nyoka na wanyama wabaya wataingia.”

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

TIBA ASILI YA UUME KUWA NA MAPELE,FANGASI NA MADONDA.

WAJUA KUWA VIAZI MVIRINGO NI TIBA.

TANGO(CUCUMBER) KATIKA TIBA NA AFYA YA MWILI.